Watu wasiookoka ambao wamezama katika
ushirikina pia wanatambua kwamba mafanikio yao huanzia katika ulimwengu
wa roho kabla hayajadhihirika katika ulimwengu unaoonekana. Wanachofanya
ni kuwaleta waganga wa kienyeji kuziweka wakfu biashara zao au miradi
yao kwa nguvu za mapepo.
Hii ndiyo njia inayowawezesha kupenya
kwa kuingia katika ulimwengu wa roho kwa kunuizia nguvu za kishetani.
Nawe mwana wa Mungu, Unaweza kupenya na kuingia katika ulimwengu wa roho
kwa kuomba katika Roho kwa kutumia mamlaka yako ya kimungu iliyopo
nyuma ya Jina la Yesu Kristo. Unapaswa kuchukua mamlaka dhidi ya nguvu
za kipepo ambazo zinapingana na mafanikio yako. Ili ushinde inabidi
uingie katika vita ya kiroho, uyaone mafanikio yako!
0 comments:
Post a Comment