Friday, 10 April 2015

MAFANIKIO YA KIMUNGU NA ULIMWENGU WA ROHO


Watu wasiookoka ambao wamezama katika ushirikina pia wanatambua kwamba mafanikio yao huanzia katika ulimwengu wa roho kabla hayajadhihirika katika ulimwengu unaoonekana. Wanachofanya ni kuwaleta waganga wa kienyeji kuziweka wakfu biashara zao au miradi yao kwa nguvu za mapepo.

Hii ndiyo njia inayowawezesha kupenya kwa kuingia katika ulimwengu wa roho kwa kunuizia nguvu za kishetani. Nawe mwana wa Mungu, Unaweza kupenya na kuingia katika ulimwengu wa roho kwa kuomba katika Roho kwa kutumia mamlaka yako ya kimungu iliyopo nyuma ya Jina la Yesu Kristo. Unapaswa kuchukua mamlaka dhidi ya nguvu za kipepo ambazo zinapingana na mafanikio yako. Ili ushinde inabidi uingie katika vita ya kiroho, uyaone mafanikio yako!

0 comments:

Post a Comment